JINSI YA KUTUNZA NGOZI YAKO KWA KUTUMIA LIMAO

Katika makala hii utapata kujua sababu mbalimbali zinazofanya watu kutokuwa na ngozi zisizokubalika. Mbali na hali ya hewa pia matumizi ya pombe, sigara , cream kali ambazo zimekuwa zikitumiwa na watu bila kujua madhara yake kumechangia kwa kiasi kikubwa tatizo hilo.
Ngozi kwa kawaida inatakiwa ijitengeneze yenyewe na si kuitengeneza kwa vipodozi kama wengi wanavyodhani. Ulaji wa matunda na mboga za majani kwa wingi kunywa glasi nane za maji kwa siku ni njia nzuri kama unataka kuwa na ngozi nzuri isiyo na madoa wala ukavu ambao haupendezi.
Wengi wanaacha kula mbogamboga na matunda kwa wingi hata kutokunywa maji ya kutosha na badala yake wamekuwa akitegemea kuwa na ngozi nzuri jambo ambalo ni gumu. Mara kadhaa tumeshuhudia watu wanaopaka cream kali wakiwa kama wameungua usoni huku uso na mwili ukionekana kuwa mkavu
Kuna watu wamekuwa na ngozi za asili na hata unapowauliza baadhi yao hawajawahi kupaka cream hata siku moja na bado wana ngozi nzuri zinazovutia hao wamekuwa wakila kwa ajili ya kuhakikisha wanatengeneza ngozi zao kutoka ndani.
Pia wengi wanaharibu ngozi zao na kuwa na madoa kutokana na kutumia make up kwa muda mrefu  na hata anapogundua kuwa ana tatizo la madoa amekuwa akijaribu kutumia cream nyingine kwa ajili ya kumaliza tatizo hilo jambo ambali linazidisha madhara kwenye ngozi.
Unaweza kutibu ngozi yenye madoa usoni  kwa kutumia limao kwa sababu ile Vitamin C iliyopo katika limao husaidia sana katika kuondoa chunusi kwa haraka.

JINSI YA KUTIBU NGOZI YAKO KWA KUTUMIA LIMAO
unachotakiwa ni kutumia maji ya limao yaliyo fresh na usiyalaze maji hayo kwa matumizi ya baadaye kisha paka sehemu zilizoathirika kila unapolala usiku. Njia hii itasaidia kukausha ngozi yako kutokana na mafuta yanayosababisha uvimbe. Asubuhi unachotakiwa ni kwenda kunawa na maji ya vuguvugu mara kwa mara, pia ijulikane kuwa  njia hii siyo nzuri kwa wale wenye ngozi laini sana.

Comments

Post a Comment

Popular Posts